Feature Image

Mzozo kati ya Trump na Papa hadharani, utamgharimu vipi kisiasa?

Mzozo kati ya Trump na Papa hadharani, utamgharimu vipi kisiasa?

Si jambo jipya kwa Rais Donald Trump kukosolewa na viongozi wa kanisa Katoliki.

Sera zake kali za uhamiaji, ambazo wafuasi wake walizikumbatia wakati wa kampeni na kuzipokea vizuri, zililaaniwa vikali na viongozi wa Kanisa.

Kwa miezi kadhaa, sera hizo zimewatenga viongozi wa kanisa Katoliki nchini Marekani pamoja na Wakristo wa kawaida.

Hata hivyo, mambo yamekuwa tofauti tangu siku chache zilizopita, pale Trump alipojipiga picha maarufu (selfie) akiwa na Papa Leo na kuchapisha picha iliyotengenezwa kwa teknolojia ya AI ikimuonyesha kama Yesu Kristo.

Jambo la kushangaza ni kwamba baadhi ya wakosoaji wake ni miongoni mwa Wakatoliki waaminifu sana na wanaofuata kwa karibu misingi ya Kanisa lenyewe.

Watu wengi hawajakerekwa tu na dhihaka ya hadharani ya Donald Trump dhidi ya Papa, bali pia hawakubaliani na vita ya Marekani dhidi ya Iran.

Hata hivyo, Vatican inaeleza kwamba kile tulichoshuhudia katika wiki za hivi karibuni si vita kati ya Papa Leo na Rais Trump, bali ni msimamo thabiti wa Papa kusimamia imani yake katika kupinga vita hiyo.

Malalamiko kuhusu jinsi Trump alivyommzungumzia Papa wa kwanza kutoka Marekani, akimwita "mvumilivu kwa watenda maovu," pamoja na picha ya AI, yamewafanya Wakatoliki wengi wa kihafidhina kubadilisha mitazamo yao tangu vita ilipoanza wiki sita zilizopita.