Feature Image

Bomu la pekee duniani linaloweza kuharibu kituo cha nyuklia cha Iran cha Fordo

Kiwanda cha siri cha Iran cha kurutubisha uranium cha Fordow kimezikwa chini kabisa ya mlima, huku vituo vyake muhimu vikilindwa na tani juu ya tani za miamba.

Israel haijaficha nia yake ya kuharibu mpango wa nyuklia wa Iran, lakini bomu pekee linaloaminika kuwa na nguvu za kutosha kupenya kituo cha Fordow ni bomu la Marekani la "bunker buster" ambalo Waisraeli hawana kufikia sasa.

Siku ya Jumatatu, maafisa kadhaa wa Israel walitangaza kuidhibiti anga ya Iran.

Jeshi la IDF lililinganisha udhibiti wa anga ya Iran na uongozi wake wa anga ya medani zingine za mzozo na maadui wanaoegemea Iran, kama vile Gaza na Lebanon - ambapo Israeli inaendelea kushambulia kwa mabomu ipendavyo.

Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu alisema siku ya Jumatatu kuwa udhibiti wa Israel wa anga ya Iran ni "ushindi mkubwa ".